
Jina lake halisi ni Deogratius Shija na pia jina hilo hilo ndilo
analofahamika nalo zaidi kwa mashabiki wake. Ni mmoja wa waigizaji
wanaofanya vizuri sana kwenye tasnia ya bongo movies nchini akiwa
ameshaigiza kwenye zaidi ya filamu kumi tofauti. Ni mwigizaji, mwandishi
na pia mwongozaji wa filamu mwenye uwezo wa hali ya juu sana.
PICHA AKIWA KAZINI.
HISTORIA YA FAMILIA
Deogratiuos Shija alizaliwa tarehe 1 mwezi wa 12 tarehe
mwaka 1978 kwenye familia yenye jumla ya watoto kumi na tano, alianza
elimu yake ya msingi mkoani Tabora katika shule ya msingi Gongoni, na
baadaye akahamia Dar es Salaam katika shule ya msingi Mwongozo ambako
alimaliza elimu ya msingi mwaka 1992, na baadaye alirudi mkoani Tabora
na kupata elimu ya sekondari katika shule ya Sekondari Uyui mjini Tabora
na baada ya hapo alijiunga na Chuo cha Foradhani jijini Dar es salaam.
HISTORIA ZAMANI.
Historia ya Deogratious shija kwenye uigizaji ilianza rasmi
mwaka 2000 baada ya kuacha kazi ya kuajiriwa kwenye hoteli ya White Sand
jijini Dar es salaam, alipojiunga na kundi la sanaa liitwalo Malongo
sanaa group lililokuwa na makazi yake maeneo ya mwananyamala, na baada
ya mwaka mmoja kundi hilo liligawanyika na shija akishirikia na Mrisho
Mpoto walianzisha kundi walilolipa jina la Dreams Art family ambalo
malengo yake makubwa yalikuwa ni kucheza ngoma na sanaa za muziki. Baada
ya kukaa na kundi hilo kwa muda, shija alipata mwaliko wa kwenda nchini
uingereza kushiriki tamasha la African Caribbean Celebration mwaka
2003, na baada ya tamasha hilo kuisha aliamua kubaki nchini Uingereza
kutafuta maisha ambako alikaa huko kwa takribani miaka minne na nusu na
akiwa huko alifanya filamu yake ya kwanza aliyoipa jina la “Lataka
moyo”, ambayo alifanya na watanzania waishio uingereza, na baadaye
alifanya filamu iitwayo “Two brothers” ambayo alifanya na marehemu Juma
kilowoko – Sajuki na mkewe Wastara Juma. Ambayo kwa maoni yake anasema
ndiyo filamu aliyoipenda sana na ndiyo iliyomuweka juu na kumtambulisha
kisanii.
Baada ya filmu hiyo alifanya filamu kama Chanzo ni mama, My
book, Aisha, Imekula kwangu, Where is God na nyingine nyingi na sasa
anajiandaa kuachia filamu yake mpya ya Lazy boy.
Akizungumzia msukomo uliomsababisha aamue kujiingiza kwenye
sanaa anasema kuwa alikuwa anakumbuka kipindi cha nyuma alipokuwa
anaangalia maigizo na anakumbuka sana jinsi ambavyo Single Mtambalike
-Richie alivyokuwa akiigiza na kumvutia na yeye kutaka kuigiza.
Akizungumzia mipango yake ya baadaye shija amesema anataka
kwenda kujiendeleza kielimu zaidi kwenye upande wa uigizaji na anasubiri
mambo yakae sawa ili aende. Pamoja na hilo pia shija amepanga kushiriki
kwenye uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015 kwa lengo la kugombea nafasi ya
ubunge kwa ajili ya kutetea wanyama na viumbe hai endapo nafasi hiyo
itaruhusiwa kwenye katiba mpya inayokuja.
0 comments:
Post a Comment