Followers

Sunday, 21 September 2014

Chekibudi msanii mahili wa filamu

 

Jina lake halisi ni Mohamed Nurdin ila kwa mashabiki wake anafahamika kama “Chekibudi”. Ni mmoja wa waigizaji wakongwe hapa nchini. Alianza kama muigizaji na sasa anatengeneza, anaongoza Filamu na pia ni mwandishi wa “script” kwa ajili yake na watu wengine. Pia ni mshereheshaji (MC) kwenye shughuli mbalimbali za sherehe. Ni baba wa watoto saba na mchezaji mzuri wa mpira wa mguu.

Picha

  • Mohamedi Nurdin (Chekibudi) 1

  • Mohamedi Nurdin (Chekibudi) 2

  • Mohamedi Nurdin (Chekibudi) 3


Historia ya familia.

 

Mohamed Nurdin alizaliwa tarehe kumi na tatu (13) mwezi wa kwanza (1) mjini Dar es Saalam katika hospitali ya ocean Road.

Alisoma na kupata elimu yake hapo hapo jijini Dar es salaam katika shule ya msingi Ilala Kasulu na baadaye akejiunga na chuo cha kiislamu, Markas Islamic kilichopo chang’ombe – Dar es salaam amabako hakumaliza baada ya kuamua kutorokea Kenya mnamo mwaka 1997 kutokana na matatizo kati yake na familia yake ambako alikaa huko kwa muda wa mwaka mmoja na nusu kabla ya kurudi Tanzania mwaka 1999.

Baada ya kurudi alipata kazi kwenye kiwanda cha azam ambako alifanya kazi kama mfagiaji na mtu wa usafi. 

Historia katika sanaa.

Safari ya chekibudi kwenye sanaa ilianzia mwaka huo huo wa 1999. Alipofukuzwa kazi toka kwenye kiwanda cha azam na kuamua kujikita kwenye kucheza mpira wa miguu. Baada ya mechi moja ya mpira wa miguu alifuatwa na Dude (mwigizaji) kumuomba akaigize nao ili kuziba nafasi ya Dr. Cheni (Mwigizaji) ambaye kwa kipindi hicho alikuwa anahama toka kundi la Splendid group na kuhamia Kaole sanaa group kutokana na mwonekano wake na pia uchangamfu wake.

Baada ya kukaa splendid kwa muda mrefu alienda kwenye kundi la nyota academia ambako alikutana na waigizaji kama Jacob steven (JB), George Tyson, Monalisa, Natasha na Single Mtambalike ambao ye mwenyewe anasema kutokana na uwezo wao wa kuigiza walizidi kumvutia zaidi kuipenda sanaa.

Filamu alizocheza ni pamoja na Sabrina, Tunu, Riyama, Machozi, out of mind, libwata, mimba, mapito na nyingine nyingi.

Akiwa nyumbani Chekibudi hupenda kukaa na watoto wake na kutazama Filamu.

0 comments: