Followers

Saturday, 30 May 2015

EATV/EARADIO YATANGAZA TIMU NA RATIBA MPYA YA PLANET BONGO

Baada ya stori kibao zilizothibitishwa na team nzima ya East Africa kupitia kupitia kipindi chake cha Planet Bongo kusema kuwa Jumamosi ya tarehe 30/05/2015 ndiyo itakuwa mwisho wa kipindi hicho kilichokuwa kinaongozwa na Abdallah Ambua na kufanya mashabiki wa kipindi hicho kutokuwa na raha baada ya taarifa hizo.

Hatimaye leo taarifa rasmi imetoka nini kitafuata baada ya kipindi hicho kufa ambacho kilikuwa kinarushwa kila siku ya Jumamosi lakini sasa Team nzima ya EATV kupitia kipindi hicho kimeamua kuwa kipindi hicho kitakuwa kinarushwa kwa siku tano kwenye wiki ambapo itakuwa ni kuanzia siku ya Jumatatu mpaka Ijumaa.

Siku ya leo katika kipindi hiki kilinoga baada ya baada ya kuudhuriwa na Dj John Dilinga, Prof Jay, Mwana Fa, Jay Mo, Enika, Mwasiti, huku Salama Jabir na Dj Kim ndiyo walikuwa wanakiongoza kipindi hicho kwa leo.

Timu mpya ambayo imetangazwa itakayo kuwa inaongoza kipindi hicho cha Planet Bongo kwa sasa ni Abdallah Ambua aka Mjukuu wa Ambua, Annah Peter, Kennedy The Remedy, Dj Ommy Crazy na Dj wa kike Sinyorita.

0 comments: