Followers

Sunday, 21 September 2014

Richie:Msanii mkongwe mwenye ubunifu.

 

Ameshawahi kupata tuzo kama Msanii bora wa kiume toka Mnet 2011-2012, na pia ashawahi kuwa finalist katika Tuzo za Egol za afrika kusini na kuwa mshindi wa pili, ni mwigizaji, mwandishi wa script, muongozaji na mtayarishaji wa Filamu, pia anajulikana kama mwanzilishi wa modern drama Tanzania.

Pamoja na mambo yote haya yeye ndiye aliyewatoa kisanii waigizaji wakubwa na wanaotamba sasa kwenye tasnia ya bongo movies kama Jacob Steven (JB), haji Adamu, John kalage,Rose ndauka  na Vicenti Kigosi (Ray). Ni baba wa watoto wawili na ashawahi kuzamia meli na kwenda msumbuji kutafuta maisha kabla ya kurudi nchini na kujikita kwenye sanaa za ya Uigizaji. Huyu si mwingine bali ni Single Mtambalike maarufu kama “Richie” kwa wapenzi wote wa Filamu nchini na duniani kote.

Picha

  • Single Mtambalike (Richie) 1

  • Single Mtambalike (Richie) 2

  • Single Mtambalike (Richie) 3

  • Single Mtambalike (Richie) 4


Historia & familia.

Richie alizaliwa tarehe tano (5) mwezi wa kumi (October) maeneo ya ilala jijini Dar es Salaam na kupata elimu yake ya msingi katika shule ya msingi Mnazi mmoja jijini Dar es salaam na baadaye. Aliweza kusoma katika shule ya sekondari Al haramain.

Kabla ya kuingia kwenye sanaa Single mtambalike alikuwa na ndoto ya kuwa baharia wa meli ili aweze kuzamia meli na kwenda ulaya ama Marekani kama ilivyokuwa ndoto ya vijana wengi wa miaka ya tisini. Katika mpango huo aliweza kupata kazi kwenye idara ya bandari. Baada ya kufanya kazi kwa muda wa kama miezi mitatu aliacha na kurudi nyumbani ambako nako alishindwana na wazazi baada ya kuwa na tabia za ukorofi sana na akaamua kuhamia kwa shangazi yake.

Baada ya muda alikutana na msichana mmoja aliyetoka uingereza ambaye alifanya ndoto yake ya kuzamia meli kuwa kweli na ndipo alipoweza pata kazi kwenye meli moja ya wagiriki na wakaondoka kuelekea  msumbiji ambako alikaa kwa muda wa mwaka miezi sita kabla ya kurudi Tanzania

Historia katika sanaa.

Baada ya kurudi Tanzania alikutana na Bishanga (mwigizaji) ambaye alikuwa fundi wa magari kipindi hicho na baadaye walikutana na waridi (mwigizaji) ambao ndo waliomshawishi kujiunga na sanaa. Hii ilikuwa ni mwaka 1997.

Baada ya kujiingiza kwenye sanaa aliweza kufanya kazi mbalimbali za Filamu zikiwemo Uyoga ,Swahiba ,Kwa Heshima Ya Penzi ,Chaguo Langu ,Tamaa Yangu,Diana ,Gentlemen ,Jesica ,Zawadi ya Birthday ,Mtaani Kwetu ,Kimya ,Basilisa ,Unexpected Truth ,Solemba ,Lerato ,The Perfect Man ,Hazina ya Marehemu ,The Stranger ,Illegal Sisters, Mahabuba

Nje ya sanaa, Single mtambalike ni baba wa watoto wawili, Prince na Darlin, na pia ni mkurugenzi mtendaji wa Kampuni yake ya Bulls Entertainment ambayo inajihusisha na marketing na promotion ya mambo mbalimbali. Ameafanya kazi na kampuni mbalimbali na ashawahi kuwa marketing and promotional manager wa kampuni ya chai kwenye mikoa ya Dodoma na Singida.

Single ni ndugu wa Msanii JB na pia ameshiriki katika kuwatoa kiugizaji wasanii wengine wakubwa kama JB, Vicenti Kigosi, Kalage, Shija,  Adam Haji, vyonne Cherry, pamoja na watu wengine maafuru kama John Kalage, John Lisa, Fatma shemweta, Mackline mdoe na wengine wengi.

0 comments: