Followers

Sunday, 21 September 2014

Kapturado:msanii mwenye uwezo wa kubadilika

 

Akiwa mmoja wa wasanii wanaofanya vizuri sana kwenye soko La bongo  movies nchini, Jina lake halisi ni Simon Mwapagata, ila kwa “fans” wake anafahamika kama Rado na kwa waigizaji wenzako anafahamika zaidi kwa jina la baba Mage kutokana na mapenzi makubwa aliyonayo kwa binti wake huyo. Ameshaigiza kwenye filamu zaidi ya kumi, na kwa sasa ni katibu wa club ya bongo movies. Kwa upande mwingine ni msanii wa muziki wa kizazi kipya (bongofleva) akiwa amefanya kazi na wasanii wachache kwenye fani hiyo. 

Picha

  • Simon Mwapagata (Rado) 1

  • Simon Mwapagata (Rado) 2


Historia & familia

Rado alizaliwa tarehe kumi na tatu (13) mwezi wa (3) huko kasulu mkoa wa kigoma na kupata elimu yake ya awali huko huko kigoma. Alianza kuonesha kipaji cha kuigiza toka akiwa shuleni ila alipendelea sana kucheza mpira wa miguu na alitaka kuwa mmoja wa wachezaji wa kimataifa lakini baadaye aliachana nao na kuamua kujikita zaidi kwenye uigizaji

Historia ya sanaa.

Ameanza kuigiza rasmi mwaka 1999 katika maigizo ya ukimwi huko tabora kabla ya kujiunga na jumba la dhahabu ambako nipo alipopata umaarufu zaidi na kujiingiza kwenye upande wa filamu.

Baadhi ya filamu alizocheza ni pamoja na Ndoto yangu, I think I hate my wife, Maduhu, Jumba bovu, Mahaba niue, Gongo la mboto, Fall in love, Nakwenda kwa Mungu , laptop n.k.

Ni mmoja wa wasanii waliioa na anaishi na mke wake jijini Dar es salaam. Anamilki gari aina ya Altezza new model.

0 comments: