Followers

Sunday, 21 September 2014

Steve Nyerere:na movie mpya 2014

 

 

MAPEMA mwezi huu, Chama cha Filamu Tanzania kilipata uongozi mpya, Steven Mengele maarufu Steve Nyerere alichaguliwa kuwa mwenyekiti akirithi mikoba ya Vicent Kigosi ‘Ray’ aliyemaliza muda wake.

Wengine waliopata nyadhifa za juu katika uongozi huo ni Makamu Mwenyekiti Mahsein Awadh ‘Dokta Cheni’, Katibu Mkuu William Mtitu na naibu wake, Devotha Mbaga huku Issa Mussa ‘Cloud’ akichaguliwa kuwa Mweka Hazina.

Kama ilivyo sehemu yoyote duniani uongozi mpya unapoingia madarakani, huweka malengo na vipaumbele vyake ili kuwawakilisha vyema wale waliowachagua.

Katika mahojiano maalumu na Mwanaspoti, Steve Nyerere alizungumzia mikakati yao mitano muhimu wanayotaka kuipa kipaumbele kuwa ni;

Kudhibiti wizi wa kazi za filamu

Suala kubwa ambalo limekuwa likiwaumiza wasanii ni wizi wa filamu, hasa unaofanywa na wachuuzi wenye vibanda vya kuuza na kutengeneza santuli ‘CD’. “Tumekosa utaratibu maalumu wa kudhibiti wizi wa kazi zetu, watu wamejifungulia vibanda wanatengeneza santuli za filamu zetu na kuziuza kwa bei chee bila ridhaa yetu.”

“Hili linatuumiza sana wasanii, hivyo uongozi wetu umepanga kushirikiana na serikali ili kudhibiti suala hilo, hatutakaa chini kamwe tukiendelea kushuhudia uhalifu huu mkubwa wa kazi zetu,” anasema Nyerere ambaye ni mwigizaji wa filamu za vichekesho maarufu komedi.

Mavazi na nidhamu

“Imekuwa ni aibu sasa, wasanii wanavaa mavazi ya ajabu na udhalilishaji hadi watazamaji wanaona aibu kutazama filamu zetu. Uongozi mpya kwa kushirikiana na wadau muhimu tumepanga kupambana na kadhia hii ili kurejesha heshima ya Bongo Movie.”

“Tunataka mtu avae kutokana na uhusika wa sehemu anayocheza, kama ni mama wa nyumbani avae kama mama wa nyumbani na kama ni changudoa avae kama changudo si filamu nzima wote wamevaa kama machangudoa,” anasema.

Ubora wa filamu

Nyerere anasema suala la ubora mdogo wa filamu za Bongo si jambo geni, filamu za Bongo zimekuwa zikifyatuliwa kama njugu, kila siku kuna filamu mpya jambo ambalo amedai hawezi kulifumbia macho

0 comments: