Followers

Tuesday, 21 October 2014

MAAJABU YA DADA ALIYEGEUKA PUNDA.

Bwana mmoja nchini Zimbabwe amedai kuwa kahaba aliyekuwa akifanya naye mapenzi amegeuka ghafla na kuwa punda.

Bwana huyo, Sunday Moyo ambaye amefikishwa mahakamani siku ya Jumatatu kwa kosa na kukutwa akifanya mapenzi na mnyama huyo amesema anampenda sana mpenzi wake huyo. Bwana Moyo aliiambia mahakama mjini Zvishavane kuwa huyo waliyemkuta naye sio punda bali ni mwanamke ambaye alikutana naye katika klabu ya usiku ya starehe.

Gazeti la Metro limesema polisi wa Zimbabwe wakiwa katika doria saa za alfajiri, walimkuta bwana huyo mwenye umri wa miaka 28, katika mji wa Mandava, akifanya mapenzi na punda nje ya nyumba yake. Mnyama huyo alikuwa amelala chini huku shingo yake ikiwa imefungwa kamba, na kamba hiyo kufungwa kwenye mti. Kwa mujibu wa mtandao wa New Zimbabwe.com bwana Moyo amekiri makosa ya kujamiiana na mnyama, lakini aliiambia mahakama kuwa "Mheshimiwa Jaji, niligundua tu kuwa ni mnyama, wakati polisi waliponikamata". Bwana huyo amesema alipata kahaba aliyekubali kulipwa dola ishirini, lakini amesema hafahamu ilikuwaje hadi akageuka na kuwa punda. "Lakini bado nampenda sana" amesema bwana Moyo. Bwana huyo ameswekwa rumande na kuamriwa kufanyiwa uchunguzi wa akili.

0 comments: