Dr Grace Mugabe na Mumewe Rais Robert
Mke wa
Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe Grace Mugabe siku hizi ni dokta, cheo
kilichozua mtafaruku nchini mwake akikinzwa katika udaktari wake wa
masuala ya sosholojia alioupatia katika chuo kikuu cha nchi hiyo,
amewatemea cheche wanaume wa eneo la Matabeleland nchini humo kuwa ni
hodari wa kuoa wake wengi kila uchao na kuwazalisha watoto na kushindwa
kuendeleza makazi yao .
Dokta
Mugabe aliyasema hayo katika mkutano wa hadhara unaokisiwa kuhudhuriwa
na watu wapatao elfu nne katika viwanja vya Gwanda mapema wiki hii.
Dokta Mugabe amewashangaa wanaume hao kutoka kabila la Ndebele kwa kuwa
maarufu wa kuzalisha na kuwatelekeza watoto bila matunzo yoyote huku
wakiendekeza ngono Zaidi.BBC
0 comments:
Post a Comment