Mwizi mmoja nchini Uchina aliyekuwa na tabia ya
kujisaidia haja kubwa katika nyumba anazofanywa wizi wake, hatimaye
amekamatwa kutokana na teknolojia ya DNA.
Polisi jijini Cixi, katika jimbo la Zhejiang
wamesema mwizi huyo aitwaye Chen mwenye umri wa miaka 29 akiwa na
mwenzake walivunja nyumba moja na kuingia jikoni na kula chakula, kabla
ya bwana Chen kujisaidia kwenye sakafu karibu na mlango.
Baada ya kufanya hayo, wawili hao wakaanza
kutafuta vitu vya kuiba ndani ya nyumba hiyo, lakini kutokana na kukuru
kakara zao, mwenye nyumba alishtuka, na wezi hao kukimbia bila ya kuiba
chochote. Miezi michache baadaye, wezi hao waliingia katika nyumba
nyingine na kuiba kompyuta mpakato-- yaani Laptop na fedha taslimu yuan
elfu moja.
Kama kawaida, waliingia jikoni na kujipakulia
chakula, na bwana chen kuacha muhuri wake wa kawaida, wa kinyesi chenye
harufu kali karibu na mlango wa mbele. Mtandao wa china daily umesema
polisi walifanikiwa kulinganisha vipimo vya DNA na mwizi Chen, ambaye
aliwahi kutupwa gerezani kwa kosa jingine mwaka 2003. Baada ya
kukamatwa, bwana Chen alikiri kujisaidia katika nyumba anazofanya wizi,
akisema, amekuwa akisoma katika vitabu mbalimbali jinsi wezi wanayokuwa
na mitindo yao ya kipekee, wanapofanya wizi. Polisi bado wanamsaka mwizi
mwenzake.
0 comments:
Post a Comment