Followers

Tuesday, 28 October 2014

UKIMWI,EBOLA VIMETENGENEZWA MAKUSUDI KUPUNGUZA IDADI YA WATU

                                                                                                                          

WAKATI DUNIA nzima ikizidi kujawa na hofu inayotokana na milipuko ya magonjwa, machafuko ya kivita, maandamano ya watu kudai mabadiliko, kuporomoka kwa maadili; majaribio ya chanjo ya ugonjwa wa Ebola yanatarajiwa kuanza kufanyika mwezi wa kwanza mwakani. Taarifa zilizotolewa na gazeti la ‘The Telegraph News’ la tarehe 22/10/2014 zinasema kwamba kampuni ya kutengeneza madawa ya Johnson & Johnson ya Marekani ndiyo iliyotengeneza chanjo hiyo ambayo inadaiwa kufanyiwa majaribio kwa wanyama na kuonyesha mafanikio makubwa. Majaribio hayo ya chanjo hiyo yatafanyika Amerika, Afrika na Ulaya.
Hii inamaanisha kwamba tatizo la Ebola limepewa muda mrefu zaidi hadi kufika mwezi Januari ili kuendeleza kukuza hofu kwa watu na kuwaandaa kwa ajili ya kukimbilia chanjo kwa haraka!
Ni kanuni gani wanayoitumia? ni kanuni ya kwanza inayosema ‘Thesis x Antithesis = Synthesis’. Wao (freemasons) wanasema: "Manufacture the crisis, then panic the people, and then step in with the solution you wanted in the first place" wakimaanisha “Tengeneza mgogoro, kisha wafanye watu wapate hofu, na kisha chukua hatua ya suluhisho ambalo ulilitaka kabla ya kutengeneza mgogoro’. Hapa mgogoro au ‘Thesis’ ni Ebola na kutokana na mgogoro huu watu wanapata ‘hofu’ ambapo suluhisho linapotolewa, yaani chanjo au ‘Antithesi’, watu wengi watakimbilia chanjo hiyo. Nini matokeo yake? Ni ‘Synthesis’ yaani kutekelezwa kwa ajenda za freemasons ambapo isingekuwa rahisi kutekelezwa kama pasingekuwepo mgogoro! Ni suluhisho gani? Kupunguza idadi ya watu duniani!
Kutokana na ukweli kwamba makao makuu ya dini ya freemasons yapo nchini Marekani, matatizo (crises) hutengengezwa Marekani ikiwa ni pamoja na suluhisho (solution) la matatizo hayo. Karibu kila tatizo kubwa linaloukumba ulimwengu wote, liwe la kiafya, kisiasa, kiuchumi au kidini, chanzo chake ni Marekani. Matatizo haya yanatengenezwa kwa lengo la kuonekana hitaji la kuanzishwa kwa serikali moja ya dunia inayodaiwa kuwa suluhisho la majanga yanayoukumba ulimwengu.
Ili kukuza matatizo, mpango unaoitwa ‘PEACE plan’ yaani mpango wa amani’ ulianzishwa. Kumbuka kwamba kila wakati mpango wowote unapoanzishwa na wafuasi wa dini ya freemasons, huweka maana mbili, moja iliyowazi, yaani ‘Exoteric meaning’ na maana nyingine ni ‘Esoteric meaning’ yaani maana iliyofichika. Kwa maana iliyowazi, PEACE Plan ni mpango mzuri wenye lengo la kuleta amani na mshikamano duniani. Lakini katika maana iliyofichika, kila herufi kwenye neno PEACE ilikuwa na maana yake. Herufi ‘P’ inasimamia lengo la ‘Plant Churches’ and Promote reconciliation’ yaani kupandikiza makanisa na kuleta mapatano. Hapa tunaona kuibuka kwa makanisa mengi katika kila kona ya dunia ambapo wengi wa waanzilishi wa makanisa hayo hupata fedha kutoka kwa wafadhili ili kutekeleza, siyo matakwa ya Mungu, bali matakwa ya wafadhili. Herufi ‘E’ ni ‘Equip servant leaders’(yaani kuweka viongozi katika serikali ambao watakuwa siyo watumishi wa wananchi bali watumishi wa wafadhili. Herufi ‘A’ ‘Assist the poor’ (kuwasaidia maskini) kama ambavyo tunaona misaada mbalimbali ikitolewa na mashirika ya kimataifa yenye lengo maalumu ndani yake; herufi ‘C’ inasimamia Care for the sick (yaani kuwajali wagonjwa ili kupunguza vifo vya watoto, kupambana na Ebola, surua, ukimwi nk) na hapa tunaona rais Obama akichukua muda mrefu kurekebisha sheria ya huduma za afya ‘health reform’ kama inavyojulikana kwa jina la  Obamacare kule Marekani, lakini lengo siyo kusaidia wagonjwa bali kusaidia kukuza ugonjwa; herufi ‘E’ Educate the next generation (kuwawezesha wanawake na usawa wa jinsia, elimu ya msingi kwa wote, na utunzaji wa mazingira) kwa ajili ya maendeleo ya kizazi kijacho. Neno PEACE linamaanisha AMANI na hakuna mtu asiyependa amani lakini neno hilo limetumiwa kama kiini macho cha kuwafanya watu wakubali mpango wa amani bila kujua lengo la mpango huo. Biblia inatuambia kwamba “Wakati wasemapo, Kuna amani (PEACE) na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafla…” 1 Wathes. 5:3.
Tayari rais Barack Obama amemteua Ron Klain kuongoza mapambano dhidi ya Ebola duniani. Hata hivyo Ron Klain ni mtu ambaye amekuwa akiona ongezeko la watu duniani kuwa ni tatizo kubwa kwa serikali za dunia. Yeye aliwahi kusema: “I think the top leadership challenge issue in our world today is how to deal with the continuing, growing population in the world and all the resource demands it places on the world and burgeoning populations in Africa and Asia that lack the resources to have a healthy, happy life,” akimaanisha kwamba ‘Nadhani changamoto kubwa ya uongozi katika ulimwengu wetu leo ni jinsi ya kutatua ongezeko la watu ulimwenguni pamoja na mahitaji yaliyopo ulimwenguni na ongezeko la watu huko Afrika na Asia linalosababisha upungufu wa mahitaji yanayotakiwa kwa afya nzuri na maisha yenye furaha’. Kwa nini Rais Obama amemteua Ron Klain kuongoza mapambano dhidi ya Ebola?  Ron Klain hakuchaguliwa kupambana na ugonjwa wa Ebola bali kupambana na ongezeko la watu ulimwenguni ambapo moja ya silaha za kufanikisha kupunguza idadi ya watu ni kutumia Ebola. Hebu tujikumbushe kile walicholenga Illuminati katika ajenda zao juu ya ongezeko la watu duniani: "Take control of the world ... to reduce ... the world to a safe level by a process of benevolent slavery and genocide ... The only alternative left to the world's ruling elite was to increase the death rate ... Dr. Aurelio Peccei of the Club of Rome ... advocated that a plague be introduced that would have the same effect as the Black Death of history." (Bill Cooper, “Behold a Pale Horse”, p. 49, 167). Bill Cooper mwandishi wa kitabu cha Behold a Pale Horse anasema kwamba idadi ya watu duniani inapaswa kuwa sawa na uwiano wa kile kinachozalishwa. Njia pekee ya kupunguza idadi ya watu ni kuongeza kasi ya vifo ambapo Dk. Aurelio Poccei wa kundi la Club of Rome aliagiza kwamba ugonjwa hatari utengenezwe ambao utakuwa na madhara sawa na janga lililojulikana kama ‘Black Death’ katika historia. Hivyo basi njia pekee ni kuongeza kasi ya vifo kuliko kasi ya kuzaliwa, (increase death rate vs birth rate). Kule China sheria inawataka wanandoa kuzaa si zaidi ya watoto wawili ili kupambana na ongezeko la watu. Hata hivyo inadaiwa kwamba kuna ongezeko kubwa la vifo ukilinganisha na ongezeko la watu kumaanisha kwamba idadi ya watu inazidi kupungua!
Sasa tujiulize swali muhimu: Je, chanjo imewahi kutumiwa kama silaha ya kupunguza idadi ya watu? Jibu la haraka ni ndiyo! Dk. Horowitz anazungumzia jambo hili katika kitabu chake alichokiita “Emerging Viruses: AIDS and Ebola.” Dk. Horowitz anatumia karibu kurasa 600 kuthibitisha kwamba Marekani kwa makusudi ilitengeneza virus vya AIDS kama silaha kisha wakaanza kuwasambaza virus hao barani Afrika kupitia chanjo zilizotolewa bure katika mpango unaojulikana kama ‘United Nations Vaccination campaign’ yaani ‘kampeni ya chanjo ya umoja wa mataifa’. Dk. Horowitz anasema yeye akiwa ni daktari mzoefu ameandika kitabu hicho akiwa anafahamu ukweli aliouandika. Hebu tumnukuu akiandika kwenye kitabu chake “Emerging Viruses: AIDS and Ebola” na hapa anasema: “Suala la kwanza lililoelezewa na Strecker ni kwamba AIDS haukuwepo Afrika kabla ya mwaka 1975, na kama ugonjwa huo ungetokana na kung’atwa na sokwe miaka ya 1940 kama inavyoelezewa, ugonjwa huo ungeonekana miaka ya 1960 na siyo miaka ya 1970. Kisha Dk. Horowitz anasema: "The World Health Organization started to inject AIDS-laced smallpox vaccine into over 100 million Africans (population reduction) in 1977. And over 2000 young white male homosexuals (Trojan horse) in 1978 with the hepatitis B vaccine through the Centers For Disease Control/New York Blood Center." [Horowitz, p. 4-5], akimaanisha kwamba ‘Shirika la afya ulimwenguni lilianza kuingiza wadudu wa AIDS kupitia chanjo ya surua kwa waafirika wapatao milioni 100 (kwa lengo la kupunguza idadi ya watu) mwaka 1977. Zaidi ya vijana wavulana 2000 wa kizungu ambao walikuwa mashoga walipewa chanjo ya hepatitis B mwaka 1978 kupitia kitengo cha kuzuia magonjwa huko New York” [rejea Horowitz: “Emerging Viruses: AIDS and Ebola” p. 4-5].
Mei 11, 1987, gazeti la London Times liliandika makala iliyoitwa “Smallpox Vaccine ‘Triggered AIDS Virus’,”  iliyoandikwa na Pearce Wright aliyekuwa mhariri wa gazeti hilo ambaye aliihusisha chanjo hiyo na mlipuko wa ugonjwa wa AIDS huko Afrika ya kati kwa sababu ndilo eneo lililokusudiwa kuanzisha ugonjwa wa AIDS na likawa eneo lililoathirika zaidi na ugonjwa huo kwa kipindi hicho. Hapa madaktari wetu wanapaswa kutusaidia kufanya uchunguzi wa kila chanjo inayoingizwa nchini kama ni salama au italeta madhara siku za usoni. Madaktari mpo?
Mwinjilist mmoja anayehubiri kwa njia ya Redio, bw. R.G. Stair, alipokea barua kutoka kwa mwanasayansi ya Bailojia (ambaye hakutaka kutaja jina lake maana alituma barua hiyo kwa siri ili mwinjilisti huyo awaambie watu). Mwandishi wa barua hiyo alisema anafanya kazi kwenye maabara pamoja na Dr. Robert C. Gallo ambaye ni mtaalamu wa bailojia ya ‘molecules’ aliyehusika katika utafiti wa asili ya virus vya AIDS. Mwandishi alisema kwamba Dr. Gallo ndiye aliyetengeneza virus vya AIDS na kuviingiza kwenye chanjo kwa nia ya kuambukiza watu. Mwandishi huyo alisema kwamba aligundua hilo alipotembelea ofisi ya Dr. Gallo na kuona barua nyingi zilizoandikwa ‘New World Order’. Kwa nini tunapata habari hizi zilizokusudiwa kuwa siri? Ndiyo! Yesu alisema: “Hakuna neno lililositirika ambalo halitafunuliwa; wala lililofichwa ambalo halitajulikana.” [Rejea Matthayo 10:26,27]; na huu ni utimilifu wa maneno hayo ya Yesu, ili kwamba tupate kujua siri za freemasons zilizokusudiwa kutuangamiza.
Mwaka 1975, Dr. Gallo pamoja na wanasayansi wengine wanane (wakiwa wanafanya kazi kwenye kituo cha utafiti wa ugonjwa wa kansa – Bethesda Cancer Research Center – huko Maryland Marekani, walifanya utafiti wa kuvifanya virus vya AIDS viweze kuambukizwa kirahisi zaidi kwa binadamu ambapo badala ya chanjo waliwezesha AIDS kuambukizwa kwa njia ya ngono kwa sababu watu wengi wanaendekeza tabia hiyo kinyume na sheria ya Mungu. Je ni wewe? Tafakari!
Mwaka huo huo, baada ya kituo cha kijeshi cha afya kiitwacho ‘Fort Detrick’ kufungwa, kilianzishwa kituo kipya kilichopewa jina la ‘Fredrick Cancer Research Facility’ kikiwa chini ya kituo cha ‘Bathesda Cancer Research Center’, ambapo Dr. Gallo alikuwa ndiye mkurugenzi wa kituo hicho. Utafiti uliofanyika mwezi Machi mwaka 1976 ulionyesha kwamba kulikuwa na kitengo cha serikali kilichokuwa kinazalisha virus vya AIDS, na kitengo hicho kilisimamiwa na Dr. Gallo pamoja na Dr. Novakhatskiy wa kituo cha ‘Ivanosku Institute’ nchini Urusi. Baadaye Dr. Gallo alipatikana na hatia katika taaluma yake lakini Rais Bill Clinton alitoa msamaha, na hivyo Dr. Gallo akawa huru.
Akijibu swali kwamba virus vya AIDS vilitengenezwa kama silaha ya kibaolojia, mwezi February, 1987, Kanali wa jeshi la Marekani David Huxsoll alisema: “Studies at army laboratories have shown that the AIDS virus would be an extremely poor biological warfare agent.” Kwamba “utafiti katika maabara za kijeshi umeonyesha kwamba virus vya AIDS ni silaha hafifu ya kibaolojia vitani.” Sasa nini kilihitajika? Bila shaka ni kutengeneza silaha nyingine ya kibaolojia ambapo Ebola ilionekana kuwa silaha yenye nguvu zaidi kwa sababu Ebola inaambukiza kirahisi zaidi kuliko AIDS!
Hebu tutulie kidogo hapa na tutafakari kile tulichokiona hadi sasa. Kwanza wanasema Marekani iliingiza mwilini AIDS kwa njia ya ‘chanjo zilizotolewa bure mwaka 1977!’ Hii inamaanisha kwamba baadhi ya chanjo za ugonjwa wa ‘small pox’ zimekuwa zikitumika kupunguza idadi ya watu wasio na hatia!
William Cooper anasema: “Whatever causes AIDS was in the Vaccine.” [rejea ‘Behold a Pale Horse’ p. 168]. Hapo anamaanisha kwamba ‘chochote kilichosababisha ugonjwa wa AIDS kilikuwa ndani ya chanjo’! Je, umepata ufunuo huo? Tafakari!
Nakushauri ndugu msomaji ujipatie nakala ya vitabu hivi viwili, “Emerging Viruses: AIDS and Ebola” cha Dk. Horowitz na “Behold a Pale Horse” cha William Cooper.
Wakati tunaelekea kuanza kuiangalia ajenda ya 36, tujikumbushe kwa ufupi ajenda ya 35 inayohusu kuanzishwa kwa serikali ya dunia katika vipengele vitano. Vipengele hivyo ni ‘A king’ yaani Mfalme, ambapo kutakuwepo na mfalme mmoja atakayetawala dunia nzima; ‘A kingdom’ yaani Ufalme ambao utakuwa umeugawa ulimwengu katika majimbo 10; ‘A seat of Kingdom’ yaani kiti cha ufalme kitakachowekwa mahali patakapokuwa makao makuu au ikulu ya serikali ya dunia; ‘A council’ yaani baraza ambapo tuliona muundo wa baraza hili ukiwa katika umbo la pembe tatu huku kukiwa na vitengo vingi vinavyofanya kazi za baraza kuu la ‘Supreme council of 13’ na mwisho tumetazama kipengele cha ‘constitution’ yaani ‘katiba’ ya serikali ya ulimwengu. Kwa ufupi hiyo ndiyo ajenda ya 35. Na sasa kuwa tayari kwa ajili ya ajenda ya 36 inayohitimisha ajenda zote za freemasons.
Usiondoke…..Itaendelea wiki ijayo
Makosa – makosa ndani ya mioyo ya watu – huchafua hisia za watu.
Kweli  –  kweli ndani ya mioyo ya watu   – hutakasa nafsi.
Mungu ni Mwema!
tafakari2010@yahoo.com

                                 Tazama news papers

0 comments: