Followers

Tuesday, 14 October 2014

WEMA SEPETU:"Nimerudi kwa nia moja tu kutengeneya filamu bora ya kisasa"

WEMA NA UJIO WA FILAMU MPYA.

 

 MREMBO na muigizaji wa filamu hapa nchini Wema Isaac Sepetu amerudi kutoka nchini Marekani na sasa yupo katika maandalizi ya filamu yake mwenyewe akiwa kama mtayarishaji na muigizaji tofauti na siku za nyuma ambapo alikuwa akishiriki katika filamu za watayarishaji wengine filamu hii ambayo bado hata jina amelificha ipo mbioni kuanza kurekodiwa wakati wowote na akiwa location ndiyo atataja jina la filamu hiyo.
Wema huku akiwa ameongozana na mchumba wake mpya kwa sasa Nassib Abdul ( Diamond) alisema kuwa safari yake ya Marekani amejifunza mengi kuhusu masuala ya filamu kwa hiyo anataka kutumia fursa hii kutengeneza filamu yenye ubora mkubwa tena ikiwa chini yake mwenyewe anajua kwa kufanya hivyo ataweza kutekeleza yale ambayo anaona ni bora kufanyika katika filamu za kisasa.

“Nimerudi kwa nia moja tu ya kutengeneza filamu bora na ya kisasa, unajua toka nimerudi kila mtu anataka kucheza filamu na mimi, lakini kwa sasa siwezi kufanya hivyo hadi nitimize ndoto zangu za kuwa na filamu yangu ambayo ni nzuri na itavutia wengi, mara nyingi nimekuwa nikishiriki filamu za watu wengine lakini sasa ni yangu mwenyewe” Alisema Wema.

Wema amefanya vizuri katika filamu ambazo aliwahi kuigiza hasa filamu yake ya mwisho ya 14 Days aliyoigiza na Jacob Stephen (JB) ilikuwa gumzo kiasi cha kila mtayarishaji kuona umuhimu wa binti huyu katika tasnia ya filamu, lakini burudani unayopata ni kwamba na mchumba wake naye inasemekana yupo katika harakati za kurekodi filamu yake naye, wanakutana katika fani au nje ya fani?

0 comments: