Followers

Tuesday, 2 December 2014

MSANII TANZA KOMEDI AFUNGA NDOA









Msanii wa sanaa ya maigizo kutoka Tanza comedy(Tanzania comedy Association),Joseph Salonge (Kamugisha),wiki hii amefunga Ndoa na mchumba wake wa siku nyingi,na aliye dai kumpenda sana.



Kamgisha ambaye pia amecheza katika sinema na Tamthiliya tofauti hapa nchini ikiwemo Milosis na Dirty Game kutoka Tuesday Entertainment. ametoa shukrani za dhati kwa wote walio fanikisha sherehe yake kufanikiwa.



Akizungumza na mwandishi wetu Kamugisha  alionyesha kuwa na furaha alipenda pia kuweka wazi ndoa yake kufuatia na baadhi ya watu kutoamini kuhusiana na ndoa yake.



“Napenda kuweka wazi kuwa kwa sasa nimeoa na wote wasio amini naomba waamini kuhusu hilo napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa wasanii wenzangu na wote waliofanikisha sherehe yangu.”



“kiukweli napenda kusema kuwa nampenda sana mke wangu...”  alisema Kamugisha



Wakati huohuo kamugisha alipenda kuzungumzia kuhusu kazi inayo tengenezwa na Mbalamwez Arts chini ya mkurugenzi Ibrahim Msuka inayo karibia kuanza hivi karibuni inayo husu Familia za kitanzania ambayo itaanza kurushwa hivi karibuni na moja kati ya vituo vya Televisheni hapa nchini.


 










 

Kamugisha kushoto akiwa amembeba mke wake baada ya kutoka kanisani.

 Kamgisha akiwa katika pozi la ufukweni na mke wake.

Habari zaidi...


0 comments: