Followers

Saturday, 9 May 2015

FRANCIS CHEKA KUPAMBA MEI 30 NA MTHAILAND

Bondia wa Fransic Cheka anatarajia kupanda ulingoni kwa mara ya kwanza Mei 30 mwaka huu tangu atoke jela. 

Cheka anatarajiwa kucheza na bondia Kiatchai Singwancha kutoka Thailand kwenye pambano la raundi kumi litakalofanyika katika ukumbi wa P.T.A Sabasaba jijini Dar es salaam.

Kaike Siraju ambaye ndiye mwaandaaji wa pambano hilo amesema kuwa amejipanga vizuri kwani kila kitu kinaenda vizuri kwa sasa ambapo mabondia wa utangulizi wote wanatarajiwa kusaini mikataba wiki hili.

Pambano hilo litasimamiwa na chama cha ngumi za kulipipwa Tanzania (TPBC) chini ya rais wake Emanuel Mlundwa. Bondia Kiatchai atawasili nchini siku tatu kabla ya mpambano huo

Credit: BBC

0 comments: